WATAALAMU WA USAFIRISHAJI TANZANIA WAWEKA SHERIA MAHUSUSI YA USAFIRI.

 WATAALAMU  WA USAFIRISHAJI TANZANIA WAWEKA  SHERIA  MAHUSUSI YA USAFIRI.


Na Mwandishi  wetu

Waziri wa  Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa   amesema kuwa  Wizara ya uchukuzi inaendelea na  hatua ya kuweka  Sheria  mahususi  ya  usimamizi wa watalaamu  wa usafirishaji nchini.

Akizungumza  Jijini  Dar es saalam Prof. Makame  mbarawa  mara baada ya   mkutano wa  chama cha watalaam wa Logistiki na Usafirishaji amesema kuwa kwa sasa wizara ya uchukuzi inaendelea kuboresha miundombinu mbalimbali ikwemo mradi wa SGR.

“ Wizara yangu inaendelea na hatua za kuwezesha kutungwa kwa Sheria Mahsusi ya Usimamizi wa Wataalam wa Usafirishaji Tanzania (Transport Professionals Registration Board Act).hivyo  Kupitia Sheria hiyo kutaanzishwa Bodi ya Usimamizi wa Wataalam wa Usafirishaji ambayo itakuwa na  jukumu  kubwa la  kudhibiti maadili na utendaji kazi wa wataalam husika. “ Alisema Prof .Mbarawa.

Aidha  Waziri Mbarawa ameongeza   kuwa Serikali  imejipanga vyema Katika  kushirikiana  na sekta binafsi ili  kuweza kutekeleza miradi kwa utaratibu wa PPP katika ujenzi wa reli mpya ya kisasa (SGR) kutoka Mtwara - Mbambabay – Mchuchuma/Liganga (Km 1000) kwa ajili ya kuendelea kuifungua ushoroba wa Mtwara.


Kwa Upande  wake rais wa chama   cha wataalam wa lojistiki na usafirishaji   Alphonce  Mingira amesema  kuwa chama hicho kinalengo la kusaidia watalaam na wafanyabiashara wa usafiri na usafirishaji Katika maendeleo ili  kuona  fursa zilizopo na  kuweka mazingira Mazuri ya utendaji kazi kati Sekta Binafsi na Serikali.

Naye  Mkurugenzi wa  idara ya Udhibiti kiuchumi  kutoka TCAA  Daniel Malanga   Amesema taasisi hiyo inaendelea  kutoa elimu kwa manufaa  ya  watanzania wote nchini.


Vilevile Mkutano huo umehudhuriwa  na Taasisi zilizopo chini ya Sekta ya uchukuzi  ambapo  washiriki kutoka wizara ya Ujenzi, Tamisemi na vyuo vya elimu ya Juu.

Post a Comment

0 Comments