Na Mwandishi Wetu, Dar es salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi Prof. Godius Kahyarara amesema kuwa Serikali imenunua vichwa nane vya Treni kati ya hivyo vichwa viwili vinatarajia kuwasili wakati wowote katika bandari ya Dar es Salaam ambavyo vitasaidia kusafirisha makasha kutoka bandari ya Dar es Salaam kwenda Bandari Kavu ya Kwala.
Kahyarara ameyasema hayo katika kikao cha wadau wa bandari kilichofanyika jijini Dar es Salaam, kikao ambacho kimezikutanisha taasisi za TRC,TRA,TPA, Wizara ya Ulinzi, Uchukuzi, Mipango na Wadau kutoka sekta binafsi.“ Serikali inaendelea kuboresha utoaji wa huduma katika bandari ya Dar es Salaam ambapo mpaka sasa imeshaagiza vichwa nane vya Treni ya kuondoshea mizigo ili viweze kusaidia kusafirisha Makontena kutoka bandari ya Dar es Salaam kwenda Bandari Kavu ya Kwala, Amesema Kahyrara.Kwa upande wake Meneja wa Bandari ya Dar es Salaam Bw. Abed Gallus amesema Uhudumiaji wa mizigo katika bandari hiyo umeongezeka sana na wanatarajia kufikia lengo walilojiwekea mwaka huu 2025/26 la kuhudumia tani milioni 32 za Mizigo.“Meli zinaendelea kuhudumiwa kama kawaida kwa ubora na kasi zaidi, kuna meli kubwa zinaendelea kutia nanga kwenye bandari ya Dar es Salaam na mizigo imeongezeka sana “ Amesema Gallus
Kwa upande wake mdau wa bandari Bw. Donald Tawalani ,Mkuu wa Kitengo cha huduma za makontena wa kampuni ya TEAGTL amesema mizigo imeongezeka hivyo ni muhimu wadau kuchukua mizigo na makontena yao kwa wakati ili bandari iweze kupata nafasi ya kuendelea kushusha mizigo mipya inayoletwa na meli.
Naye Mwenyekiti wa TATOA Bw. Rahim Dossa ameomba Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari na Wakala wa Barabara (TANROAD) kujenga mizani katika eneo la Bandari Kavu ya Kwala ili kuondoa usumbufu kwa madereva wa Malori.










0 Comments